Na Omary Mbaraka
Hivi karibuni taasisi yetu ya habari ilitembelea KAMPUNI ijulikanayo SINORAY MOTERCICLES inayojishughulisha na vitendea kazi muhimu ambavyo vinaongeza ajira hapa nchini pikipiki za miguu mitatu au kwa jina maarufu Guta ambazo hupakia abiria pia mizigo
Kampuni hii ambayo ipo Kariakoo jijini Dar es salaam na mkoani pwani Ina wafanyakazi mia tatu na inamilikiwa na watu wenye asili ya kichina
Kampuni hii hujishughulisha na uundaji (assemble) wa pikipiki za aina zote yakiwemo aina ya Sinoray nk
Meneja mkuu wa kampuni hii bw Alex Lii alisema kampuni hii inafuata taratibu na sheria zote za serkali kwa wafanyakazi ikiwa ni pamoja na kuwalipa wafanyakazi kima cha serkali, kupima afya zao, kujiunga na " Workers Compensation Fund "(WCF) kulinda afya zao pakitokea ajali,pia mikataba na kuwapa vitendea kazi huku meneja mwajiri bw Raphael akionyesha vitendea kazi vingi vilivyohifadhiwa stoo






0 Comments