Na Omary Mbaraka
Kwani ni ukweli hivi sasa Afrika inahitaji sana sauti ya hekima na juhudi za dhati katika kujenga amani, hivyo uteuzi wake unaonesha imani kubwa iliyowekwa juu yake katika kusimamia diplomasia ya kuzuia migogoro, kuimarisha mazungumzo jumuishi ya kisiasa na kujenga uaminifu miongoni mwa wadau mbalimbali.
Hakika, uwezo wake wa kutafuta suluhisho bunifu na endelevu ndio msingi hasa katika kipindi hiki ambacho Afrika inahitaji sana sauti ya hekima na juhudi za dhati katika kujenga amani, uteuzi wake unaonesha imani kubwa iliyowekwa juu yake katika kusimamia diplomasia ya kuzuia migogoro, kuimarisha mazungumzo jumuishi ya kisiasa na kujenga uaminifu miongoni mwa wadau mbalimbali.
Uteuzi huu ni ushahidi wa wazi wa hazina yake adhimu ya uongozi, uzoefu mpana wa kidiplomasia, pamoja na uadilifu na busara alizoendelea kuzionesha kwa miaka mingi katika ngazi za kitaifa, kikanda na kimataifa. Ameendelea kuwa kielelezo cha kiongozi mwenye maono, utulivu wa fikra na uwezo wa kuunganisha watu kwa ajili ya pamoja
Aidha, tunatambua na kuthamini umahiri wake wa kuratibu wadau wa kimataifa na kikanda wakiwemo "Intergovernmental Authority on Development, East African Community, League of Arab States" pamoja na United Nations katika kuleta mshikamano, ufanisi na mwelekeo mmoja wa juhudi za kulinda amani na usalama wa kikanda.
Taasisi hii ya habari inamuombea afya njema, MHE Kikwete na hekima zaidi na nguvu ya kuendelea kukabiliana na changamoto zilizopo, huku akisukuma mbele ajenda ya amani ya kudumu, ustawi na maendeleo ya Bara letu.




0 Comments