Blog Post

WAFANYAKAZI KATIKA KAMPUNI ZA WAPO HATARINI

 Na Mwandishi wetu 

 Afya za wafanyakazi katika kampuni hizi zipo mashakani kwani wanafanya kazi katika mazingira magumu ikiwemo maji machafu yanayotokana na kusafisha bidhaa ambazo ni uume wa ng'ombe

Kampuni hizi ambazo zinamilikiwa na raia wa china anaejulikana kwa  jina la mama U na mwanawe Allan zinanunua na kusafirisha nchi za nje uume wa ng'ombe 

Hata hivyo waandishi  wa chombo hiki Cha habari walipotembelea eneo lao la kazi maeneo ya kiwalani maarufu" Kwa Guru"walielezwa kuwa wakurugenzi hawapo ambapo baadhi ya wafanyakazi walithibitisha kuwa wamefanya kazi kwa muda mrefu kati ya miaka miwili Hadi mitatu wakiwa ni vibarua jambo ambalo ni kinyume Cha sheria

Pia wafanyakazi hao walionekana wakiendelea na kazi katika Hali ya uchafu huku hawana vitendea kazi pia walikili kutembelewa na taasisi mbali mbali za serikali lakini mazingira  ya kazi zao hayabadiliki Bado ni magumu

Post a Comment

0 Comments

Close Menu