Blog Post

MBUNGE CHALINZE AHUISHA TAARIFA ZAKE DAFTARI LA MPIGA KURA




 Na Omary Mbaraka 

Mbunge wa Jimbo la Chalinze na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-anayeshughulikia masuala ya Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Mhe Ridhiwani Kikwete Jana amejitokeza katika Ofisi ya Kata ya Msoga kwa ajili ya kujiandikisha na kuboresha taarifa zake katika Daftari la kudumu la Mpiga kura ili aweze kupata fursa ya kuchagua viongozi kwenye uchaguzi.

Mhe Kikwete ametumia fursa hiyo pia kuhamasisha wananchi wengine kujitokeza kujiandikisha au kuboresha taarifa zao ili haki hii muhimu ya kupiga kura isiwapite. Zoezi hili limeanza tarehe 13 Februari na litaisha Februari 19, 2025 kwa mkoa wa Pwani na Tanga, na hivyo kuwataka wananchi kutumia fursa hii kwa siku hizi. Akizungumza baada ya kukamilisha zoezi la kuweka taarifa zake sawa, Mh. Kikwete aliwahimiza wananchi kujitokeza huku akisifu uharaka wa uandikishaji na waandikaji walivyo na spidi ya kujiandikisha na ushirikiano wanaotoa kwa wanaokuja kujiandikisha.

Zoezi hili la uandikishaji pamoja na kuandikisha wapiga kura wapya lakini linalenga kuboresha pia taarifa za wapiga kura wa zamani wakiwemo wale waliopoteza kadi zao . Zoezi linakwenda vizuri na wananchi wanaojitokeza wamekuwa wengi hata kuvuka malengo ya kusajiri kwa siku.

Post a Comment

0 Comments

Close Menu