Blog Post

MHE NCHIMBI NA MHE KIKWETE WASHIRIKI MKUTANO WA TAPSEA ARUSHA


 Makamu wa Rais Mhe Nchimbi na Waziri wa utumishi ofisi ya RAIS Mhe Ridhwani Kikwete wameshiriki ufunguzi wa Mkutano wa 13 wa Chama Cha Waandishi Waendesha Ofisi -TAPSEA kilichofanyika Ngurdoto, Arusha.


Mkutano huo ambao ulifunguliwa na Mgeni Rasmi Balozi Dr. Emanuel Nchimbi, Makamu wa Rais wa JMT umewakutanisha Wana-TAPSEA takriban 5050 toka Serikali zote na Halmashauri zote pamoja na taasisi mbalimbali toka Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar. Akizungumza katika mkutano huo Makamu wa Rais, Dr. Nchimbi amewahimiza wajumbe wa mkutano huo ambao utatimia kwa kuchagua uongozi mpya wa Chama Chao kuzingatia haki na kwamba waepuke masuala yote yatakayo kipotezea uelekeo chama chao.


Nikizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, nimewakumbusha wanataasisi hao juu ya juhudi kubwa zinazofanywa na serikali kuhakikisha kuwa wafanyakazi nchini wananeemeka na matunda ya serikali yao kwa kuwakumbusha kuwa tumepandisha madaraja ya watumishi, tumebadili muundo na vyeo, tumelipa madeni ya mishahara nk. Na pia tumeahidi kuendelea kufanya hivi katika bajeti hii ya mwaka na kuendelea kila panapopatikana bajeti.

Post a Comment

0 Comments

Close Menu