Humphrey Herson Polepole ni mwanasiasa na mwanadiplomasia ambaye ni balozi wa Tanzania nchini Cuba alichaguliwa tangu 2023. Alikuwa balozi wa Tanzania nchini Malawi kuanzia 2022 hadi 2023.
Habari za kijamia
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan akiwa katika ukaguzi
Na Omar Mbaraka
Pamoja na mafanikio makubwa yanayoonekana katika stendi ya mabasi yaendayo kusini mwa Tanzania,inayosimamiwa na asasi ijulikanayo Umoja wa Mabasi yaendayo kusini mwa Tanzania ( UMAKUTA).
Mwenyekiti wake kwa niaba ya asasi hio anaiomba halmashauri ya Temeke kushiriki kusaidiana katika kuboresha miundo mbinu ya stendi hio.
Akiongea na Tafakari news Weblog kaimu Mwenyekiti wa UMAKUTA bw Kiboko alianza kwa kuelezea mafanikio mengi ya stendi hio ikiwa ni pamoja na utulivu na kuwatendea haki wasafiri wa kusini mwa Tanzania lakini kubwa ameiomba halmashauri ya Temeke chini ya mkurugenzi wake Elly huruma washirikiane na asasi yao kuboresha miundo mbinu ambayo ni chakavu sana
Bw Kiboko alisema kwa vile stendi hio inaipatia pia mapato mazuri halmashauri hio ya Temeke hivyo ni wazi kuwa miundo mbinu ikiboreshwa mapato pia yataongezeka katika hamashauri yetu ya Temeke hivyo ni muhimu kwa halmashauri hio kuweka umuhimu wa kuboresha
Hivyo basi bw Kiboko ameomba kikao cha pamoja na mkurugenzi wa Temeke
Kaimu mwenyekiti huyo bw Kiboko amesema stendi hio ambayo ipo Mbagala rangi tatu pia inachangia fedha nyingi katika serikali kuu kupitia kodi mbalimbali za TRA zikiwemo pia kutoka kwa wafanyabishara
Wanao miliki fremu nyingi za biashara katika stendi hio
Bw Kiboko ambae ana kaimu nafasi ya mwenyekiti aliefariki wiki hii alisema asasi yao imesajiriwa kisheria hivyo hivi karibuni watafanya mkutano mkuu cha kumthibitisha kuwa mwenyekiti kwa mujibu wa katiba ya UMAKUTA
Post a Comment
0
Comments
Social Plugin
TAFAKARI MEI 15, 2025
UTULIVU
UTULIVU WA KIPEKEE NDANI YA HOTELI YA KITALII YA NASHERA
Ndani ya hoteli ya Nashera
Miongoni mwa hoteli zilizoko karibu na mbuga ya wanyama ya Ruaha na Mikumi iko katika mji wa kiserikali Dodoma na mji wa kibiashara Ikulu ndogo Dar es salaam ndani ya hoteli hiyo kuna utulivu wa aina yake
0 Comments