Blog Post

MBAGALA NI KITUO KIKUU CHA KUCHENJUA MCHELE NA SUKARI

 Na Omar S Mbaraka 

Utafiti unaoendelea kufanywa na chombo hiki cha habari umegundua kuwa maduka mengi makubwa ya kuuza bidhaa kwa jumla yaliopo maeneo ya Mbagala rangi tatu ndio vituo vikubwa  vya kihalifu vya  kubadili ("Re bagging ")vifungshio kutoka halisi na kuweka vya bandia ili mradi bei iongezeke ama kufanikisha kuuza bidhaa isio na ubora

Ni bidhaa nyingi zinazofanyiwa mchezo mchafu huo lakini zaidi ni sukari na mchele.  Maduka hayo ambayo yanamiliki maghala makubwa hubadilisha sukari iliotoka  Brazil ambayo iliingizwa hapa ncini kwa msamaha wa kodi uliotolewa na serikali ili kukidhi mapungufu yaliojitokeza ya sukari hapa nchini na kuwekwa katika vifungashio vya sukari kutoka mtibwa na hivyo kuuza kwa bei ya juu

Pia kwa upande wa mchele wafanyabiashara hao huufanyia ukarabati mchele mbovu ikiwa ni pamoja na kuupakaza mafuta ili unukie na kuonekana mchele bora kutoka kyera mbeya na maeneo mengine na hivyo kuuzwa kwa bei ya juu

Hata hivyo tulipoongea na mtoa habari wetu alisema wafanyabiashara hao wamekuwa wakikamatwa lakini wanaachiwa na wanaendelea na shughuli zao  jambo ambalo licha ya wananchi kulishwa mchele mbovu pia wanauziwa bidhaa hizo kwa bei ya juu baada ya kubadili vifungashio

Post a Comment

0 Comments

Close Menu