Blog Post

RAIS MSTAAFU WA AWAMU YA PILI MZEE ALLI HASSAN MWINYI AFARIKI DUNIA


Na   Omar Mbaraka

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo Februari 29,2024  kwa  masikitiko makubwa ametangaza kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi kilichotokea saa kumi na moja na nusu katika Hospitali ya Mzena Jijini Dar es salaam.


Rais mstaafu Mzee Ali Hassan Mwinyi hapo awali alilazwa London kwa matibabu na baadae kurudishwa hapa nchini na kulazwa katika hospitali ya Mzena jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu ya Saratani ya Mapafu hadi umauti ulipomfika leo Februari 29,2024

Aidha Mhe Rais Dkt Samia kufuatia taarifa ya msiba huu mzito ametangaza siku saba za maombolezo na bendera kupepea nusu mlingoti kuanzia kesho

#PumzikakwaamanimzeeMwinyi.
 

Post a Comment

0 Comments

Close Menu