![]() |
Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiao wa Afrika Mashariki |
Na Omar Mbarak
Kongamano kubwa la maboresho ya sera ya mambo ya nje linatarajia kufanyika mwezi huu kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali kutoa maoni yao.
Kwa mujibu wa mwaliko wa kushiriki kongamono hilo uliotolewa kwa
wadau mbalimbali na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
kongamano hilo litahusu Maboresho ya Sera mpya ya Mambo ya Nje ya mwaka 2001
Kongamano hilo litashirikisha wadau mbalimbali kutoa maoni kuhusu maboresho ya
Sera Mpya ya Mambo ya Nje ya mwaka 2001 na Mkakati wake wa Utekelezaji.
Kwa mujibu wa wizara hiyo kongamano hilo litakalofanyika katika
Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es
Salaam tarehe 9 Januari, 2024 kuanzia saa 3.00 asubuhi.*
Wizara hiyo imetoa wito kwa wadau na kuwaalika wadau wote ikiwa ni pamoja na;
Wanachuo/Wasomi, Wanasiasa, Vyama vya Siasa, Taasisi za Kidini, Asasi za
Kiraia, Taasisi Zisizo za Kiserikali (NGOs) na wananchi kwa ujumla kushiriki
Kongamano hilo muhimu litakalosaidia kukusanya maoni yatakayowezesha kupata
Sera imara ya Mambo ya Nje.*
0 Comments