Blog Post

KUHIMIZA AJIRA ZA BODABODA BILA MAFUNZO NI KUCHOCHEA UMASIKINI NA KUPUNGUZA NGUVU KAZI YA TAIFA



Na Omar Mbaraka

Hivi karibuni Mkurugenzi aliyemaliza muda wake Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI), alisema kuwa asilimia sabini ya wagonjwa waliolazwa wodi za taasisi hiyo wanatokana na ajali za pikipiki maarufu kama bodaboda.

Hivyo basi kutokana na  taarifa hiyo ya kushtua ilipelekea kwenda kuwatembelea majeruhi wa ajali katika hosptali ya MOI, lengo kubwa lilikuwa ni kuwapa pole na kujua kulikoni!

YALIOJITOKEZA

Kati ya wagonjwa wa majeruhi wa ajali za bodaboda niliobahatika kuwatembelea katika taasisi  ya MOI baadhi walikuwa ni abiria na wengine walikuwa ni madereva wa bodaboda.

Baadhi ya majeruhi tayari wamekuwa wamepata ulemavu wa kudumu hata baada ya kuruhusiwa kutoka hosptali atakuwa akitembelea magongo au baskeli ya walemavu (wheelchair),  jambo ambalo hatoweza kufanya kazi tena zaidi ya kuwa tegemezi kwa familia na Taifa kukosa nguvu kazi

Baada ya kufanya utafiti wangu mdogo nimegundua kuwa ukiukwaji wa sheria kama vile kupakia abiria zaidi ya mmoja, maarufu kama mshikaki na kukimbia mwendo kasi, pikipiki inapakia watu wanne jambo ambalo linasababisha dereva wa bodaboda kukosa balance na hivyo kusababisha ajali. Pia huku wakikiuka sheria za barabarani kwa kupita wakati wa taa nyekundu

Kutokana na kukiuka sheria za barabarani madereva wa bodaboda wamekuwa wakisababisha seriakali badala ya kupoteza nguvu kazi ya mtu mmoja iwapo atapakia abiria mmoja akipata ajali, sasa badala yake inapoteza nguvu kazi ya watu wanne kwa kupakia mshikaki.

Utafiti unaonesha kuwa kuna baadhi ya bodaboda hufunga honi za magari makubwa, jambo ambalo limekuwa kero kwa wananchi na linaweza kuwa sababu ya magonjwa ya shinikizo la moyo kuongezeka na kusababisha presha na mshutuko kwa watu kwani honi hizo zimekuwa zikipigwa bila mpangilio barabarani.

Honi hizo za magari makubwa zinazofungwa na dereva wa bodaboda zimekuwa kero kubwa sana baadhi ya dereva wa bodaboda wakifika karibu na magari hupiga honi hizo na kushtua dereva wa gari akidhani kuwa kuna gari kubwa linakuja nyuma yake na hivyo kujaribu kulikwepa na matokeo yake kusababisha ajari.

Madereva wa bodaboda wanaofunga honi hizi wanakiuka kanuni kwa sababu wataalam waliotengeneza bodaboda hizi hawakufunga honi za magari makubwa kutokana na matumizi ya vyombo hivyo havistali kuwa na honi kubwa zenye kushtua watu.

USHAURI

Neno la bodaboda limetokana na nchi ya jirani ya Uganda lina maana ya ‘boarder to boarder’ likiwa na maana ya mpaka hadi mpaka, hivyo basi tafiti zinaonesha kuwa baadhi ya nchi jirani kama vile Uganda na Rwanda madereva wa bodaboda wanapewa mafunzo ya usalama barabarani na wanaongoza kwa kutii sheria za barabarani  na hivyo ajali katika nchi hizo zimepungua sana.

Pamoja na ukweli kuwa usafiri wa bodaboda ni muhimu na unasaidia kupunguza tatizo la ajira hapa nchini, hivyo viongozi wanatakiwa kuhimiza bodaboda kuchukua mafunzo ya usalama barabarani, kutii sheria za barabarani, pia  plate namba za bodaboda ziwe na rangi maalum ili askari wa usalama barabarani iwe rahisi kudhibiti bodaboda za kupakia abiria. Hivyo badala ya viongozi kuhimiza ajira za bodaboda badala yake pia wahimize madereva wa bodaboda kupewa mafunzo kwanza ya sheria za barabarani 

Kuedelea kuhimiza bodaboda kama njia ya kuongeza ajira kwa vijana bila kutoa mafunzo ya usalama barabarani na kutii sheria inapelekea kusababisha kuongezeka kwa umaskini katika familia kutokana na familia nyingi kuwaghalamikia majeruhi mamilioni ya shilingi na  kupoteza nguvu kazi ya Taifa kwa ajali za bodaboda ambazo zinazidi kuongezeka kila kukicha

 

 


Post a Comment

0 Comments

Close Menu