Blog Post

BILIONI 39 KUSABABISHA CHUKI KWA SERIKALI YA RAIS S DKT SAMIA

 

Na Omar Mbarak

Wakala wa Ufundi na Umeme Nchini (TEMESA), inazidai taasisi mbalimbali za serikali zaidi ya shilingi bilioni 39 na hivyo kushindwa kuzilipa kampuni binafsi za wazawa zilitoa huduma kwenye taasisi mbalimbali za serikali.

Kutokana na uchunguzi uliofanywa na blog hii unaonesha makampuni mbalimbali ya binafsi yalitoa huduma mbalimbali zikiwemo za kusambaza vifaa mbalimbali zikiwemo nyanya za umeme, zinaidai TEMESA zaidi ya bilioni 39.

Kutokana na taasisi mbalimbai za serikai kushindwa kuilipa TEMESA kwa wakati, TEMESA inashindwa kuwalipa wazabuni hao kwa wakati na hivyo kusababisha malalamiko kwa wazabuni na chuki kwa serikali yao.

Mwandishi wa habari hizi alipoongea na baadhi ya wafanyabiashara waliokuwa wakifuatilia madeni yao Makao Makuu ya TEMESA jijini Dodoma, baadhi wanasema kuwa wana hofu ya kufilisiwa na benki ambazo walikopa mikopo baada ya kushindwa kurejesha mikopo yao kwa wakati kutokana na malipo yao kuchelewa kwa muda mrefu baada ya kutoa huduma kwenye taasisi za serikali.

Wanasema kutokana na kushindwa kulipwa malipo yako kwa wakati baadhi yao watoto wao wamekatisha masomo kwa kujiunga na vyuo  hivyo hatua ambayo inapelekea kuanza kujenga chuki na serikali yao lakini hawana la kufanya.

Mfanyabishara mmoja ambaye ni Kada wa Chama cha Mapinduzi CCM ambaye hakupenda kutaja jina lake, anasema kuwa serikali ni mali ya  CCM na watendaji wa taasisi za serikali wanaosababisha uzembe huu wa kuchelewesha malipo yao yanaweza kupelekea kura kwa CCM wakati wa uchaguzi ujao kupungua.

“Deni la bilioni 39 ni kubwa na linajumuisha na kuhusisha familia nyingi,” anasema Kada huyo wa CCM.

Hivyo amezitaka taasisi hizi za serikali ambazo zilipewa huduma na makampuni binafsi kulipa mapema TEMESA ili iweze kuwalipa wadai wake.

Majukumu ya msingi ya TEMESA ni kufanya matengenezo ya Magari, pikipiki na Mitambo ya Serikali katika Karakana ambazo zipo kila Mkoa

Kufanya matengenezo na Usimikaji wa Mifumo ya Umeme, Mabarafu, viyoyozi na Elektroniki, Kufanya matengenezo ya taa za kuongozea magari (Traffic Signals) na taa za barabarani (Street Lights)

 

Kukodisha magari kwa ajili ya usafiri wa Viongozi (VIP Vehicles) yaliyopo katika Kitengo cha GTA (Government Transport Agency) ;

Kukodisha mitambo ya kuzalisha kokoto, na mitambo ya kazi za barabara;

Uendeshaji wa Vivuko vya Serikali; Kutoa ushauri wa Kitaalamu kwa Serikali na Umma kwa ujumla katika nyanja za uhandisi wa Ufundi, Umeme na Elektroniki; utoa ushauri wa kitaalamu kuhusu usimikaji wa mifumo mipya ya uhandisi wa Ufundi, Umeme na Elektroniki; na

Kufanya usanifu na Usimamizi wa usimikaji wa mifumo ya uhandisi wa Ufundi Umeme na Elektroniki ili kukidhi viwango vinavyotakiwa na kwa kulingana na matakwa ya Sheria na Taratibu zinazoongoza taaluma husika.

 

 


Post a Comment

0 Comments

Close Menu