Vizazi vyao wametumia miongo kadhaa kutafuta mabaki hayo na hivi majuzi, katika kile kinachoitwa ugunduzi wa miujiza, mafuvu mawili ya watu waliouawa yametambuliwa kati ya mkusanyiko wa maelfu ya vitu vya kale.
Ugunduzi wao unaunganisha pamoja hadithi ya ukatili wa kikoloni, kampeni kali na matumizi yasiyokuwa ya kawaida ya utafiti wa DNA.
Ni nadra kupata mti wa mshita kwenye miteremko ya chini ya Mlima Kilimanjaro.
Matawi yake yanayopinda-pinda hufika juu ya barabara yenye mwinuko na kusimama nje kati ya mimea minene yenye rutuba.
Wakati fulani, ilifunika soko la wanakijiji wa Tsudunyi, sehemu ya kule ambako sasa kunajulikana kama Old Moshi, walikofurahia hali ya baridi kali iliyotokana na eneo la juu zaidi.
Lakini eneo hilo muhimu katika jamii likawa janga kubwa na licha ya amani kutokana na mazingira asilia, sasa athari zake zimerejea miongo kadhaa baadaye.
Ilikuwa hapa tarehe 2 Machi 1900 ambapo, kama wazao wanavyosema, mmoja-mmoja wale watu 19, wote wakuu au washauri, walinyongwa.
Walikuwa wamehukumiwa kwa haraka siku moja kabla, wakituhumiwa kupanga njama ya kushambulia majeshi ya Ujerumani.
Madai ya Ujerumani kwa sehemu hii ya bara yalirasimishwa katika Mkutano wa Berlin wa 1884-1885.
Mataifa ya Ulaya yaligawanya Afrika kabla watu wanaoishi huko kutoa maoni yoyote juu ya kile kilichotokea.
Mangi Meli, au chifu mashuhuri zaidi kati ya wale waliouawa, mwaka 1892 alifanikiwa kuwashinda wanajeshi wa Ujerumani.
Mafanikio hayo yalibadilishwa baadaye na kufikia mwisho wa Karne ya 19 Ulaya ilikuwa na nia ya kuleta ushawishi katika sehemu hii iliyojulikana kama Ujerumani ya Afrika Mashariki.
0 Comments