Na Omary Mbaraka
"Karibu ukimbie wakati huohuo ukisaidia kuboresha huduma ya Afya ya Mama na Mtoto." Mhe Ridhwani Kikwete
Baada ya Msimu wa kwanza wa MSOGA MARATHON kufanikiwa sana mwaka Jana 2024, Sasa Jumatano Agosti 30, 2025 ni Msimu wa pili. Mbunge wa Jimbo la Chalinze mkoani Pwani Mhe. Ridhiwani Kikwete kwa kushirikiana na Viongozi wenzake wanaendelea na MSOGA MARATHON kwa ajili ya kukimbia wakati huo huo kuchangisha fedha ili kwenda kuboresha huduma za Mama na Mtoto.
Kutakua na Km 5, Km 10 na Km 21 na itafanyika Msoga Grounds Chalinze. Jisajili sasa kupitia Mtandao wa YAS tukaokoe maisha yao
0 Comments