Blog Post

MASHIRIKIANO KIPINDI CHA MAJANGA YAWEKEWA MIKAKATI-WAZIRI KIKWETE

 






Na Omary Mbaraka 

Waziri wa kazi ajira vijana na wenye ulemavu ofisi ya waziri mkuu Mhe Ridhwani Jakaya Kikwete amefanya kikao kazi na  viongozi kutoka Wizara ya Katiba na Sheria wakiongozwa na Mkurugenzi Msaidizi Huduma za Kisheria kwa Umma,  Abdulrahman Mohamed Msham, Taasisi ya OSHA wakiongozwa na Mtendaji Mkuu wa OSHA,  Khadija Mwenda pamoja na  viongozi wa Chama cha Msalaba mwekundu Tanzania  (Tanzania Red Cross Society ).

Kikao hicho kimefanyika tarehe 12 Mei 2025 jijini Dodoma. 

Katika kikao hicho kwa pamoja wamejadili na kuelekeza kuimarisha  mashirikiano ya kazi katika kipindi cha majanga. Pia Mhe Kikwete amewapongeza kwa utayari wa viongozi wa pande zote kuhakikisha maslahi ya Wananchi yanakuwa ya kipaumbele. 



Post a Comment

0 Comments

Close Menu