Na Mwandishi wetu
Kauli ya askofu Rweyongeza ya kuitaka serikali ibane wimbi la manabii na mitume wanaozidi kujitokeza hapa nchini aliyoitoa katika jubilee ya askofu Rwoma katika Jimbo la katoliki Kayanga imeungwa mkono na wengi
Askofu Rweyongeza amesema ni wakati muafaka bunge na serikali kurekebisha ibara ya 19 (1) na (2) ya katiba yetu ya nchi ambayo inatoa uhuru wa kuabudu na kuhubiri dini na kufanya ibada kwa uhuru bila kuingiliwa na serikali matokeo yake wapo watu wamejitokeza na kujiita manabii au mitume bila uzioefu Wala kusomea wakiwa na malengo ya kujitajirisha,
Askofu Rweyongeza amekemea miujiza ya uongo ya kuwaponya watu na akasema kama kweli Wana uwezo waende katika ICU ya mahospitali wawaponye wagonjwa
Mwandishi wa habari pia amekutana na wananchi kadhaa ambayo wanaunga mkono kauli ya askofu Rweyongeza ambapo bw Jacob Ngaiza nae amesema kama kweli hawa manabii Wana uwezo wangeenda muhimbili wodi ye yote kama vile Mwaisela wawaponye wagonjwa wote waliolazwa waondoke warudi majumbani bw J Ngaiza alisema watu wanaozidi kutiwa umasikini kwa kuwalaghai kutoa sadaka na kununua maji ama mafuta ambayo hayasaidii cho chote na baada ya kutiwa umasikini huo wanalaumu serikali ya mama dk Samia.
Nae Eliza Christian amesema yupo nabii mmoja hakumtaja jina anakwenda mikoani kuwachukua watu na kuwafundisha jinsi ya kuwa walemavu na akifika katika mahubiri anajifanya kuwaondolea ulemavu huo na mlemavu wa ukweli asipoponywa anamusmbia Bado Hana Imani kubwa kwa mwenyezi mungu hivyo aongeze ibada
Hivi karibuni makamu wa Rais Dk Philip Mpango huko Arusha amemuagiza waziri wa mambo ya ndani kupitia idara ya usjiri kupitia vyema usjiri wa makanisa
Na hivi karibuni serikali ilifuta usajiri wa kanisa la Christian Life na miliki wa kanisa Hilo bw Dominic K Dibwe mzaire aliejiita Kiboko ya Wachawi kufukuzwa nchini
Nae Imma Shango yeye anajiuliza kuwa serikali Ina vyombo vizuri vya ulinzi na upelelezi sijui inashindwaje kugundua udanganyifu mkubwa katika makanisa haya ambapo viongozi wake wamejilimbikizia Mali nyingi kwa udanganyifu
0 Comments