Humphrey Herson Polepole ni mwanasiasa na mwanadiplomasia ambaye ni balozi wa Tanzania nchini Cuba alichaguliwa tangu 2023. Alikuwa balozi wa Tanzania nchini Malawi kuanzia 2022 hadi 2023.
Habari za kijamia
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan akiwa katika ukaguzi
Mei 3 kila mwaka Dunia huadhimisha siku ya ya Uhuru wa Vyombo vya Habari, ambapo uhalisia unaonesha hali ya Vyombo vya Habari si nzuri kimaudhui, kifedha, na kiteknolojia.
Na ili kuepuka kufikia hali mbaya zaidi ni wazi kuwa Vyombo vya Habari vinatakiwa viwekeze kwenye teknolojia na waandishi kuongeza ujuzi, ili kuendana na wakati huku fedha ikitafutwa sambamba na serikali kuunga mkono kwa kuvipatia matangazo vyombo vyote vya habari kwa usawa kwani ni ukweli kwamba asilimia 80 ya mapato ya vyombo vya habari hutokana na matangazo.
Aidha, sote tunatambua ujio wa uchaguzi wa Serikali za mitaa kwa mwaka huu 2024 na uchaguzi mkuu wa 2025, katika hili Vyombo vya Habari vinatakiwa kutoa nafasi sawa kwa vyama vya siasa katika kuripoti matukio mbalimbali.
Nchini Tanzania maadhimisho haya pia yanafanyika na kwa siku ya kwanza Spika wa Bunge, Tulia Ackson alikuwa mgeni rasmi na alikazia kwa kusisitiza ufuatiliaji wa taasisi za serikali zinazodaiwa fedha na vyombo vya habari, ili walipe madeni yao na vyombo viweze kujiendesha.
Leo Mei 3, 2024 ni kilele cha siku hii muhimu kwetu, mgeni rasmi ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, tunataraji kuna jambo ataliongea ingawa tayari Waziri mwenye dhamana ya Habari Nape Nnauye amesema jambo.
Namnukuu, “hali ya uhuru wa vyombo vya habari katika nchi yetu inaendelea kuimarika, hatujafika tunakotaka kwenda lakini kwa hakika hatupo tulipokuwa jana, mazingira ya jana na leo ni tofauti na wanahabari wanakubaliana na mimi, tumefika hapa kwenye maboresho haya yaliyofanyika kwa sababu ya utashi wa kisiasa wa serikali.”
Pia katika siku hii ya kuadhimisha uhuru wa habari Tafakari news Weblog inalaani vikali mauaji ya waandishi wa habari wapatao ishirini na mbili na wengine kushikiliwa na majeshi ya Israel katika vita vinavyoendelea Gaza
Post a Comment
0
Comments
Social Plugin
TAFAKARI MEI 15, 2025
UTULIVU
UTULIVU WA KIPEKEE NDANI YA HOTELI YA KITALII YA NASHERA
Ndani ya hoteli ya Nashera
Miongoni mwa hoteli zilizoko karibu na mbuga ya wanyama ya Ruaha na Mikumi iko katika mji wa kiserikali Dodoma na mji wa kibiashara Ikulu ndogo Dar es salaam ndani ya hoteli hiyo kuna utulivu wa aina yake
0 Comments