Blog Post

MAHAFALI YA KUMI NA SABA YAFANYIKA MUHIMBILI


Novemba 2 2023 yalifanyika mahafali ya kumi na saba katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), ambapo madaktari katika fani mbali mbali walitunukiwa diploma na digrii

Katika mahafali hayo ambayo yalifana sana mkuu wa chuo Rais mstaafu wa Zanzibar Mhe Abeid Amani Karume ndie alietunuku shahada hizo kwa madaktari wa fani mbalimbali wakiwemo madaktari bingwa.

Mmoja wa wahitimu aliewakilisha wahitimu wa shahada za awali bw Whitefrank M Frank katika hotuba yake alisema  nanukuu "Kwa wazazi na walezi wetu, leo tumetimiza ahadi ya uaminifu kwenu na fani hizi zikawe zawadi kwenu kwa kujitoa kwenu kuhakikisha tunapata urithi bora wa elimu.Zaidi ya yote tunarudisha sifa na shukurani kwa mwenyezi mungu  kwa kutupa  nafasi ya kufanya haya.

 Hivyo basi jana ilikuwa pia ni furaha kwa wazazi wa madaktari hao kama uonavyo katika picha hapa chini  Mzee Omar Mbaraka na bi Zuhura Abdi wakiwapongeza watoto wao Dr Abdallah Bakari Shekhalage kuwa daktari bingwa pua, koo na masikio(Otorhinolaryngologist/ENT Surgeon) na Dr Warda Omary  Mbarak kupata masters of Radiology  (Radiologist)

o


Post a Comment

0 Comments

Close Menu