Na Mwandishi Wetu
Marieta Banga, ambaye alipoteza watu wanane wa familia katika maporomoko ya matope Wilaya ya Hanang Kaskazini mwa Tanzania anasema hakuna kilichosalia, bado ana uchungu.
Banga anasema, "Tulisikia kelele nyingi, tukakimbilia nje, tukaona matope na mafuriko. Baadaye, baada ya mvua kuacha, tulikwenda kutazama upande wa juu na kuona hakuna nyumba iliyobaki...
“…hakuna kilichosalia, na watoto wetu wote walikuwa wamekwenda. Watoto wa kaka yang, sita kati yao na mama yao pia walikuwa wametoweka. Jamaa mwingine ambaye tunakaa naye hayupo, na kufanya jumla ya watu wanane. Walisombwa na mafuriko makubwa,” anasema Banga.
Mvua kubwa iliyonyesha mwishoni mwa juma ilisababisha maporomoko ya matope katika eneo la Katesh huko Hanang, na kuathiri mamia ya watu.
0 Comments