
Na IBRAHIM KADILO
Kabla ya
kuamua kurusha tagazo lako kwenye mitandao ya kijamii, unatakiwa kuzingatia
mambo ya msingi ili kuweza kufanikisha kufanya mauzo mtandaoni kwa urahisi
zaidi bila kutumia nguvu nyingi.
Katika
makala haya ntakueleza jambo moja la msingi sana kabla ya kurusha tangazo lako
unalotakiwa kuzingatia katika biashara yako ni kuchagua walengwa wako sahihi wenye
matatizo sugu yanayosumbua.
Kabla ya
kuendelea mbele nieleze kwa ufupi target
market ni nini? Hili ni kundi fulani la watu wenye mahitaji yanayofanana,
mfano fikiria upande wa afya na urembo, hili ni eneo pana sana katika soko,
saloon ya urembo inaweza kutoa huduma za aina mbalimbali.
Kama vile kukata
kucha, kufanya make up, massage nk. Kwa
mfano tukichukua moja katika ya huduma hizo za saloon kama kufanya massage.
Hiyo ndio linakuwa
target market yetu au kwa jina
lingine ndio niche yetu tunaweza kuongeza zaidi kujipambanua kwa kutoa massage
kwa wanaume.
Hilo ni
kundi la watu ulilolipambanua vizuri unaweza kufikiri kwa nini tunajiweka
kizuizi kwenye soko kwa sababu fedha zetu za kufanya marketing hazitoshi kama
utalenga soko pana zaidi ujumbe wa kuwafikishia walengwa wako utakuwa dhaifu.
Pia lengo la
matangazo yako ni kwa walengwa wako (prospects), ili kuona tangazo lako na
kusema “waoo hili ni kwa ajili yangu”
Hii ndio
maana unahitaji kuchagua soko lako lengwa kwa kuwa kila kitu kwa kila mtu
inapelekea suala zima la marketing kushindwa kufanya kazi.
Hii haimaanishi
huwezi kutoa huduma kwa wengini, elewa kuwa tunajiainisha na huduma lengwa kwa
ajili ya kufanya kampeni katika marketing iwe rahisi.
Kujaribu
kumlenga kila mtu inamaanisha kuwa haujamlenga mtu yeyote, kwa kuwa na soko
pana unaua namna ya kujitofautisha na washindani wako na hivyo kuua kabisa mkakati
wa masoko.
Jinsi ya kuchagua walengwa wako?
Baada ya
kuelewa umuhimu wa kuchagua target market
kabla ya kurusha matangazo yako kwenye mitandao ya kijamii, sasa ni wakati wa
kuchagua soko lako lengwa, ebu tuangalie mfano wa mpiga picha anavyoweza
kuchagua soko lake lengwa.
Mpiga picha
anaweza kuwa anatoa huduma za kupiga picha za harusi, picha za makampuni, picha
za waandishi wa habari, picha za familia, hii ni aina pana sana ya soko la
picha. Njia nzuri ya kufikiria jinsi ya kuchagua soko lako lengwa ni kutumia
kanuni ya PVP Index.
PVP index ni ( Personal fulfillment, Value to the
marketplace and Profitablility), yaani
katika kanuni hii unaangalia Kulidhika kwako wewe binafsi kwa kutoa huduma hiyo
kwa kundi la watu fulani, kuna watu huwa wanafanya kazi wasizozipenda kwa
sababu ya fedha.
Personal
fulfillment unaangalia kiwango cha kulidhishwa kwako kutoa huduma hiyo, kiasi
gani unafurahi kushughulika na hao watu.
Value to the
marketplace, unafanya tathimini ya huduma hiyo unayotoa kwenye soko hilo kwa
kiasi gani soko hilo linathamini kazi yako.
Profitability unaangalia kiwango cha faida kwa
kutoa huduma hiyo kwenye soko kinalidhisha ni chenye faida.
Kwa mfano
mpiga picha anaweza kuchagua soko lake lengwa
kama ifuatavyo:
Kwa kutoa
huduma ya kupiga picha za harusi Personal fulfillment akajipa alama 5, Value
akajipa alama 7, kwenye profitability akajipa alama 9 jumla ya alama 21.
Kwenye kutoa
huduma ya picha za makampuni Personal fulfillment akajipa alama 3, value
akajipa alama 6, profitability akajipa
alama 9 jumla ya alama 18.
Kwenye kutoa
huduma ya picha za waandishi wa habari Personal fulfillment akajipa alama 9,
value alama 7, profitability alama 2
jumla ya alama 18.
Kwa kutoa
huduma ya picha za familia Personal fulfillment akajipa alama 9 value akajipa
alama 8 na profitabilty akajipa alama 9 jumla ya alama 26.
Hapa walengwa wa mpiga picha huyu ni wale
wanaohitaji picha za familia kwa sababu ndio kazi anayoifurahia yenye faida na
inathamani kubwa kwenye soko kuliko zingine.
Hii
haimaanishi kuwa huwezi kushughulikia soko lingine bali juhudi zetu za kufanya
masoko zitajikita kwenye soko letu lengwa zaidi.
Punde tutakapo dhibiti soko hili ndio tunahama kwenda kwenye soko lingine hivi ndiyo unaweza kuchangua soko lengwa na kufanikiwa katika kufanya mauzo mtandaoni.
Kupata mafunzo zadi ya bure ya jinsi ya kufanya biashara mtandaoni tuma ujumbe whatsapp namba 0744499499 utaunganishwa kwenye group la whatsapp.
0 Comments