Blog Post

CHALINZE WAPOKEA GARI LA ZIMAMOTO


 




Na Mwandishi Wetu, CHALINZE


HALMASHAURI ya Wilaya ya Chalinze mkoani Pwani, wamepokea gari la Zimamoto na Uokoaji punde yanapotoke majanga hayo wilayani hapo toka kwa Mrakibu Mwandamizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (SSF) Jenifa Shirima.

Akiongea kwa niaba ya wananchi wa Chalinze, Mbunge wa jimbo la Chalinze Ndg. Ridhiwani Kikwete amemshukuru Mrakibu Mwandamizi huyo kwa niaba ya serikali kwa kuona kuwa katika mipango ya serikali Chalinze nayo iwe moja ya maeneo ya kipaumbele katika uhitaji wa gari hilo.

 Mbunge alikumbusha kilio cha muda mrefu cha wananchi wa Chalinze na majanga yaliyowahi kuwakuta na kusema ujio wa gari hilo ni ukombozi mkubwa.

Akizungumza kabla ya kumkabidhi Mbunge wa jimbo hilo, Mrakibu Mwandamizi Jenifa alimpongeza Mbunge kwa kuwasemea wananchi wake na kusema gari hilo ni utekelezaji wa maombi ya Mbunge Kikwete.

Mrakibu alimuahidi Mbunge huyo ambaye pia ni Naibu Waziri wa Utumishi na Utawala Bora kuendelea kutatua kero za zimamoto katika halmashauri zote mkoa na kwamba na pia kumshukuru Mkurugenzi mtendaji wa Chalinze kwa kuwapatia Kiwanja ambacho watajenga Jengo la zimamoto la wilaya na ofisi zao.

Pia alimuhakikishia Mbunge kuwa serikali inajipanga kwa ajili ya ujio wa gari kubwa wilaya hiyo.

Wananchi wa Chalinze kwa jumla yao wameishukuru Serikali kwa kutatua kero hiyo ya muda mrefu na Wameahidi kulitunza gari hilo.  

Post a Comment

0 Comments

Close Menu