Blog Post

CHATANDA APOKEA WAPINZANI 114 KATIKA WILAYA YA BUKOBA




Na Mwandishi Wetu, Bukoba

MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi  (UWT) Ndg. Mary Chatanda  amewapokea  wanachama 114 kutoka vyama vya upinzani katika Kata ya Katoro wilayani  Bukoba Mkoani Kagera  ambao wameona juhudi kubwa ya   Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika kuleta Maendeleo makubwa katika Taifa.

Mwenyekiti Chatanda amewapokea Wapinzani hao jana katika ya Katoro na kusema matunda ya Rais Samia ndio yamefanya Wapinzani ndani ya wilaya ya Bukoba  kuhamia CCM hivyo akawaomba  viongozi wangu kuwapa ushirikiano mzuri katika kuhakikisha Chama cha Mapinduzi kinaendelea kukua zaidi .

"Nimefurahi kupokea wanachama wapya katika wilaya hii ya Bukoba maana kurudi kwa wapinzani sisi CCM ndio chachu ya kuongeza wanachama wapya katika wilaya yenu muwape ushirikiano wa kutosha kwa Maendeleo ya Chama chetu", amesema. 

Post a Comment

0 Comments

Close Menu